Jumamosi, 19 Oktoba 2019

ZOGOLO MAKUNGANYA NO. 2 ZOGOLO MAKUNGANYA.

Ukoo wa Zogolo











Zogolo Makunganya alikuwa ni mtu mwenye asili ya maumbile ya watu wa zamani, umbo lake lilikuwa kubwa; ni mwenye urefu wa Ft 6.30. Upana wa kutoka bega la kulia kwenda bega la kushoto ni sm 20. ana muonekano wa kifua kipana; yaani ni pandikizi la jitu.
Alikuwa ni mtu mwenye nguvu nyigi,   Rangi ya ngozi yake ilikuwa ni ya maji ya kunde.
Baada ya kuzaliwa Kisaki; makuzi na maisha yake yalimpeleka katika kijiji cha Madimla, hicho ni kipindi cha karne ya 19 takriban miaka ya 1900.
Alipokuwa Madimla aliweza kupata kizazi; yaani familia, lakini hata hivyo baada ya utawala wa kikoloni Zogolo aliitelekeza familia yake kutokana na hisia za kuwa utawala wa kikoloni uliotawala kanda hiyo wakati huo hautaacha kumsumbua,
alitoroka na kwenda kujichimbia katika kijiji cha Mngeta; huko alianza makazi mapya ambapo alijichukulia mke na kuzaa watoto wakiwemo Mwinyimkuu Zogolo na Sefu Zogolo.                Rehema Zogolo, Nuru Zogolo-{Tozi}            Zakia zogolo, Kisamvu Zogolo.
Mwisho wa maisha yake yalikuwa hapo hapo Mngeta Visima Saba. Akiwa ameacha watoto akiwemo Sefu Zogolo.
                         nakala ya mwaka 1927.
imehifadhiwa na kulindwa na wazee wa kale wa ukoo huu.
_________________________________________________________________________________

KARIBU PWANI YETU

ZOGOLO MAKUNGANYA NO.8 ZOGOLO, MATAMBO, MBONDO NI NDUGU MOJA KOO MBALIMBALI.

  ZOGOLO, MATAMBO, MBONDO NI NDUGU MOJA KOO MBALIMBALI. Mlaluhombo alikuwa na mdogo wake waliozaliwa kwa mama mkubwa na mdogo, huyu mdogo al...