Jumatatu, 16 Mei 2022

ZOGOLO MAKUNGANYA NO.8 ZOGOLO, MATAMBO, MBONDO NI NDUGU MOJA KOO MBALIMBALI.

 


ZOGOLO, MATAMBO, MBONDO NI NDUGU MOJA KOO MBALIMBALI.

Mlaluhombo alikuwa na mdogo wake waliozaliwa kwa mama mkubwa na mdogo, huyu mdogo aliolewa na bwana mmoja mwenye asili ya kijiji cha Disunyala kijiji kilichopakana na mji wa Mlandizi mkoa wa pwani nchini Tanganyika,  jina la mzee huyo lilitambulika kuwa ni Kondo lwinde, Kondo lwinde alizaa na mama huyo watoto wafuatao:-  Ally Kondo, Salumu Kondo na binti kondo watatu, lakini binti kondo hawa watatu; mkubwa wao alipata bahati ya kuolewa na mzee mmoja aitwae Shomvi Pazi na kuzaa nae mtoto aitwae Hazimala binti Shomvi, na baada ya hapo binti Kondo huyo aliachwa na kuolewa na mwanamme mwingine aitwaye Mohammedi Mbondo, hapa ndipo walipozaliwa Selemani mbondo, na mwingine aitwaye binti Mohamedi (King’amba),

Kwa msingi huu Hazimala binti Shomvi, na Selemani mbondo pamoja na binti Mohamedi (King’amba) hawa wote ni ndugu moja kutoka katika tumbo la binti Kondo mkubwa; lakini wakiwa baba zao ni mbalimbali.

Kati ya ndugu hawa; huyu aliyeitwa Hazimala binti Shomvi; alipata bahati ya kuolewa na mzee aitwae Kondo Matambo, ambapo alizaa nae watoto sita. wakwanza ni bi Mwajuma binti Kondo, wa pili ni Jumane Kondo, wa tatu ni Amini Kondo, wanne ni Stumai Kondo (mama Sele),   wa tano ni Asha Kondo (mama bovu), wa sita ni Pili Kondo. Asili ya Kizazi hiki unapokichunguza utaona kinatokea katika tumbo la mdogo wake Mlaluhombo; ambapo huyu Mlaluhombo ndiye  mama mzazi wa Mintanga Sefu, Selemani Sefu, Hadija Sefu, Athumani Sefu, Ally Sefu, na Chambuso Sefu. Watoto hawa walipatikana baada ya Mlaluhombo kuolewa na Sefu Zogolo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KARIBU PWANI YETU

ZOGOLO MAKUNGANYA NO.8 ZOGOLO, MATAMBO, MBONDO NI NDUGU MOJA KOO MBALIMBALI.

  ZOGOLO, MATAMBO, MBONDO NI NDUGU MOJA KOO MBALIMBALI. Mlaluhombo alikuwa na mdogo wake waliozaliwa kwa mama mkubwa na mdogo, huyu mdogo al...